Friday, 18 May 2018

MAKONDA ATOA ONYO KALI KWA WANAWAKE

Na Shani Seif

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amewaonya wasichana wa mkoa wake wa Dar es salaam kutokubali kuolewa na wanaume wanaoishi katika maeneo ya bondeni ambayo ni hatarishi hasa katika kipindi cha mvua za masika.



Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam


Makonda amesema hayo alipofanya ziara katika eneo la mbagala kiburugwa na kuona baadhi ya nyumba za wananchi ambazo zimeathirika kutokana na kujengwa katika maeneo hatarishi na kuwataka wakazi hao kuhama mara moja.

Makonda ameongeza kuwa serikali  haitaweza kutoa msaada wa chakula na malazi kila mara kwa wananchi ambao wanakumbwa na majanga yanayotokana na wao kuamua kukaa katika maeneo hatarishi kwa kujitakia.




Baadhi ya wakazi wanaokaa mabondeni

Mkuu wa mkoa huyo amedai kuwa maeneo hayo ni ngumu kwa mwananchi kupata msaada wa dharura ikiwemo gari la wagonjwa au huduma ya zima moto.

Yanga kukupiga na rayno sport leo

Na Pamela chamafwa

Baaada ya kupokea kipigo kizito cha mabao 4-o dhidi ya kikosi cha sumlalyer ya nchi Algeria.








kikosi cha wana jangwani leo tarehe 
15/2/2018 wanachuana leo dimbani kukipiga dhidi ya kikosi cha rayor sport cha nchini Rwanda katika mchezo wa pili hatua ya makundi.

MAJALIWA ATOA AGIZO KUHUSU MAFUTA

Na. Pamela chamafwa
Dar es salaam.

Waziri mkuu wa jamhuri  ya muungano wa Tanzania mh.kassimu majaliwa amehitimisha mjadala wa kuwataka wafanyabiashara  wote hapo nchini kuingiza mafuta hayo sokoni ndani ya saa 72 .
Majaliwa ametoa agizo hilo baada ya spika wa bunge joh ndungai kuitaka serikali kueleza ufumbuzi wa tatizo la kuadimika kwa mafuta na kukwama kwa meli za mafuta bandarini kutokana na tatizo la kodi.

Waziri mkuu Kassim Majaliwa


Kwa upande wake waziri wa viwanda biashara na uwekezaji Charles mwaijage amesema mahitaji ya mafuta nchini ni kati ya tani laki 4 hadi 4 na nusu kwa mwaka huku vyanzo vya mafuta hapa nchini ikiwa ni asilimia 30 pekee.

WANAFUNZI WAJITOKEZA KATIKA ZOEZI LA KUPIGA KURA

Na Shani Seif

Mchakato wa Uchaguzi   unafanyika siku hii ya leo katika chuo cha Uandishi wa habari cha TIME SCHOOL OF JOURNALISM TSJ . Wanafunzi chuoni humo wanafanya zoezi  la kupiga kura la kuchagua viongozi ngazi ya Urais na makamo wa urais.

Uchaguzi umesimamiwa kikamilifu na walimu ,mwenyekiti wa tume pamoja na viongozi ukizingatia usalama na utulivu wa wanafunzi kufanya zoezi hilo bila vurugu.


Mmoja wa wanafunzi akipiga kura
Wanafunzi wakijiandaaa kupiga kura

Chumba cha kupigia kura


Aidha wanafunzi wameonekana wakifanya zoezi hilo la kupiga kura kwa utulivu huku wakiwa na shauku kubwa ya kusubiri matokeo ambayo yanatolewa siku hii ya leo baada ya zoezi la kupiga kura kukamililka

WATU WAWILI WANUSURIKA KATIKA AJALI


Na Shani Seif

Ajali mbaya imetokea asubuhi  hii leo  majira ya saa moja  kaika  Barabara ya Al  Hassan mwinyi eneo la sayansi. Barabara hiyo ambayo ipo katika matengenezo  na bado haijakamilika




Polisi wakiwa wanachunguza ajali


   Wadada wawili wamejikuta gari lao Escudo likigeuka lilikotoka na kuwa miguu juu mbele kabisa la jengo la kituo cha sheria na haki za binadamu  na kupata majeruhi madogo madogo  na mmja wake kukimbizwa hospitali kwa kupata huduma ya kwanza



Gari aina ya Escudo likiwa limepinduka

Mmoja wa majeruhi (kushoto) alienusurika katika ajali hiyo




Thursday, 17 May 2018

IJUE KAULI MBIU YA SIKU YA MAMA 2018

NA AMINA SANGAWE


Siku ya kimataifa ya mama Duniani ilianzishwa rasmi mwaka 2009 na umoja wa mataifa nahuadhimishwa kila mwaka April 22 ili kutoa nafasi ya kuthamini umuhimu wa mama katika hii dunia.
Siku hii maalum kwa kina mama duniani huambatana na kauli mbiu ambayo kwa mwaka huu ni’’SITISHA UCHAFUZI WA MAZINGIRA PLASTIKI’’.kauli hii imetokana na waraka wa Baba mtakatifu Fransisko usemao’’Ujumbe huu ambao umesheheni  mapokeo ya kidini pamoja na ushauri wa kisayansi unaweza kufanyiwa kazi katika ngazi mbalimbali kuanzia kwa watu binfsi,vyama vya kiraia,serikali na mashirika ya kimataifa ili kukuza na kuimarisha mchakato wa maendeleo endelevu,usawa na kuzingatia haki za msingi kibinaadamu.
Siku ya mama duniani huadhimishwa nan chi nyingi ikiwemo Tanzania ,Lengo kuu la kuadhimisha hii siku ni kwaajili ya kumshukuru mama wa familia,pamoja na umama,uzazi wanaopitia pamoja na mchango wao mkubwa katika jamii


MASELE APANDA CHEO


NA AMINA SANGAWE.

Mbunge wa shinyanga mjini kwa tiketi ya CCM,Stephen Masele amechaguliwa kuwa makamu wa Rais wa Bunge la  Afrika [PAP].

Taarifa hiyo imetolewa mei 11 mwaka huu Bungeni Mjini Dodoma  na mwenyekiti wa Bunge,Andrew Chenge na kubainisha kuwa mbunge huyo kijana amechaguliwa mei 10 mwaka huu.

Cheng amemsifu mbunge huyo kwa utendaji wake mzuri wa kazi na kuongea ‘’umelipa Bunge letu sifa na Tanzania kwa ujumla.Nafasi hii  ni ya kuitangaza nchi yetu na Bunge hili na tunamtakia kazi njema huko aendko.



UDART YISHTAKI SERIKALI


NA AMINA SANGAWE


Kampuni ya mradi wa usafirishaji ya mabasi ya mwendo kasi[UDART]imefungua kesi mahakamani dhidi ya serikali kupinga kitendo cha kuletwa mwekezaji mpya.

Hatua ya serikali kutafuta mwekezaji mwingine imetangazwa Mei 10 mwaka huu na Waziri  MkuuKasim Majaliwa akiwa Bungeni baada ya kampuni hiyo kuonekana kusuasua katika utendaji wa mradi huo.

Bila kusahau kampuni ya Udart imewahi kufunguliwa kesi ya madai mahakamani na kampuni ya Maxam wiki tatu zilizopita kwa kushindwa kulipa gharama za uendeshaji,uwekezaji na haki stahiki za wafanyakazi.


UCHAGUZI WATIKISA CHUO CHA UANDISHI TSJ

Na. Pamela chamafwa  
Dar es salaam .
Zoezi  la uchaguzi wa serikari  ya wanafunzi katika chuo cha uandishi wa habari  Tsj  limeendelea kuwa pasua kichwa baada ya kampeni  za wagombea kupamba moto

Wagombea watatu wana chuana vikali katika nafasi ya uraisi  na wagombea wa wili katika nafasi ya umakamu wa urais wanao shiriki katika nafasi ya Rais ni Kulwa Karedia Jacton, Abdulrahman Kinana, na Rashidi Rashidi huku nafasi ya makamu wa uraisi ikiwaniwa na  Aisha Charlse pamoja na Mohamed Ng’oula




Badhi ya wanafunzi  chuoni hapo akiwemo Richard Deo wamesema nivigumu kutabiri ni mgombea gani atakae weza kuibuka mshindi kutokana na kampeni zinazoendelea


Zoezi hilo la uchaguzi litahitimishwa may 18 ambapo wanafunzi wote watajumuika kupiga kura ili kuwachagua rais na makamu wa rais kama ilivyoanishwa na tume ya uchaguzi chini ya mwenyekiti odrian niclous  

NA :KHADIJA M HASSAN

  • MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA JIJINI 

Hivi ndivyo hali ilivyokatika maeneo meng jijini dar es salaam kutokana na mvua zinazo endelea kunyesha
kwa mujibu wa mamlaka ya ha li ya hewa imesema kua mvua zinazozidi milimeta 50 kwa saa 24 itaendelea kunyesha katika maeneo ya ukanda wa pwani ikiwemo dar es salaam na visiwa vya unguja na pemba hali hiyu inatokana na kuimarika kwa ukanda wa mvua
Hai ni kama ilivyo njia hazipitiki

baadhi ya nyumba za kinondoni kwa msisiri zikiwa zimezungukwa na maji kila pembe

UCHAGUZI WAPAMBA MOTO TSJ



              

Na Juliani Salvatory

    Uchaguzi wa serikali ya Wanafunzi Time School of Journalism umezidi kupamba moto hii ni baada ya wagombea wa nafasi ya Uraisi chuoni hapo kuendelea na shughuli za kampeni za kunadi sera zao kwa wanafunzi.

Uchaguzi huo unao talajiwa kufanyika siku ya ijumaa ya Tarehe 18-5-2018, unaonekana kuwa na maswal mengi kuhusu nani hatakayeibuka mshindi katika uchaguzi huo hii ni kutokana na wagombea kuwa na sera nzuri za kimaendeleo katika chuo hiko.
Habari Picha-

Mgombea wa nafasi ya Uraisi Rashid Hassan akizungumza na baadhi ya Wanafunzi mapema leo chuoni hapo.

Mgombea wa nafasi ya uraisi Rashid Hassan akiwa katika moja ya darasa chuo hapo akiendelea na shughuli za kampeni.

mgombea wa nafasi ya Uraisi Rashid Hassan katika,akiwana kampeni manager wake kushotoni Edwadi Benson wakati kulia ni Neema Edisoni.

Wednesday, 16 May 2018

MVUA ZAWA GUMZO JIJINI DAR ES SALAAM


           


  Na Juliani Kasimiri

  Mvua zinazoendelea kunyesha katika mkoa wa Dar es salaam zimeonekana kuwa gumzo kubwa hii ni kutokana na mvua izo kunyesha mara kwa mara,nakupelekea athari kubwa kwa wakazi wa mkoa huo hususani wa maeneo ya mabondeni
Mvua hizo zinatakribani wiki moja tokea zianze kunyesha katika maeneo mengi mkoa humu,lakini zimeonekana kuwa na athari kubwa za kiuchumi na kimiundombinu.
Hussain Bakari ni mfanyabiashara katika soko la buguruni,kwa upande wake mvua hizo zimemfanya ashindwe kufanya biashara zake za kupanga mboga mboga hii ni kutokana na kunyesha mara kwa mara kwa mvua hizo.


Asha Mussa ni mkazi wa buguruni yeye anaona mvua hizo zimefanya usafiri kuwa mgumu hususani anapotaka maeneo yake ya kazi kuelekea nyumbani.

Ata ivyo watu mbali mbali katika mkoa huo wameonekana kuendelea na shughuli zao za kujipatia kipato,licha ya mvua hizo kuendelea kunyesha katika maeneo mengi jiji hapa.