Wednesday, 16 May 2018

WAKANDARASI WA BARABARA WALIA NA MAMANTILIE


Na Gladness Mapesa

WAKANDARASI wa eneo la Ubungo Kibangu Jijini Dar es salaam walalamika wafanyakazi wa  eneo hilo hususani maman’tilie kwa kuuza  vyakula katika mazingira yasio salama



Wakizungumza na UMOJA BLOG mmoja wa wakandarasi hao Maiko Ally alisema  kutokana na mvua za masika zilizoanza kunyesha maeneo mbalimbali, wamekuwa wakipata chakula hicho katika mazingira machafu  jambo ambalo linaweza kuleta mlipuko wa magonjwa hususani kwa gonjwa la kipindupindu katika eneo hilo

Ally alisema kuwa kutokana na hali hiyo wanawaomba wafanyabiashara hao kuwauzia chakula hicho katika mazingita safi

“Sisi  wakandarasi wa eneo hili tunawaomba mamantilie wanaotupikia chakula katika eneo hili  waboreshe mazingira ya kufanyia kazi zao za uuzaji wa vyakula kwani mazingira ni machafu na hutupa wakati mgumu sisi walaji na wengine hula wakiwa wamesimama ”alisema  Ally

Mmoja wa wauzaji wa vyakula eneo hilo aliyejitambulisha kwa jina la  Imelida Peter  anaandaa chakula  katika sehemu safi na salama titizo ni kwa wakandarasi wenyewe hutumia eneo hilo kwa haja ndogo pindi waendeleapo na kazi zao.

“siuzi chakula katika mazingira machafu mimi naandaa chakula change katika sehemu safi na salama titizo ni kwa wakandalasi wenyewe hokojoa katika eneo hilo pindi waendeleapo na kazi zao na wengine kutoa hata haja kwa pembeni ya eneo hilo kwani lipo kalibu na kichaka”

“ Mkandarasi mkuu ndio aliyeniomba mimi kuwapikia chakula ili kuokoa muda wao kwenda mbali kufuata chakula”alisema Imelida

UMOJA BLOG  lilizungumza na  Mkandarasi Mkuu wa eneo hilo yeye alijitambulisha kwa jina moja  la Thomas ambapo alisema alikubali mazingira wanayotumia kwajili ya  chakula  sio salama na yeye ndio alimuomba mama uyo awe  anawapikia chakula

“ Kwaupande wa mazingira machafu tatizo lipo kwa wakandarasi wenyewe sio maman’tilie huyo kwani  wengi hao wamekuwa wakitoa haja zao karibu na eneo hilo la kupatia chakula

UMOJA BLOG  ilipojaribu kumtafuta mwenyekiti wa eneo hilo ili kuweza kutolea ufafanuzi suala hilo lakini  hakuweza kupatikana





0 comments:

Post a Comment