Wednesday, 16 May 2018


Na;Neema Edson
20171017_173426%257E2

Wakazi wa yombo kilakala wilayani Temeke mkoani Dar es salaam wachoshwa na uchafunzi wa mazingira utokanao na viwanda katita mto yombo ambao husababisha uchafunzi wa mazingira pamoja na uchafunzi wa bahari ya hindi kwakua maji hayo hutiririka kuelekea baharini
.
Mmoja wa wakazi katika eneo hilo Bw. Seif Chekwa amezungumza na Umoja blog na kusema kuwa mto huo umekua ukichafuka kutokana na maji machafu yanayo toka viwandani kutiririshwa na kuelekezwa katika mkondo wa mto huo jambo ambolo huchafua mto huo na mazingira kwa ujumla.
Aidha Chekwa amesama maji hayo hutoa harufu mbaya ambo nikero kwa wakazi wanao zunguka mto huo jambo ambalo ni hatari kwa afya ya wakazi hao pamoja na watoto wadogo wanacheza katika maji hayo machafu.

Mbali na hayo Chekwa  amedai kuwa kutokana na uchafuzi huo unasababisha ongezo la mbu katika eneo hilo ambao huambukiza ugonjwa wa maralia kwa kiasi kikubwa ingawaje watu wanajitahidi kujifunika vyandarua nyakati za usiku wanapo lala.

Vilevile mto huo awali  ulikua ukitumika katika shughuli mbalimbali zinazo wasaidia wakazi wa eneo hilo kama kuchota maji ya kutumia majumbani pamoja na shughuli za kilimo cha mbogamboga katika mashamba yaliyopo katika mbonde la mto huo hivyo shughuli hizo zimekatishwa kutokana na uchafuzi huo.

Pia Chekwa ameiomba serikali kuingilia kati suara hilo ili kukomesha tatizo hilo na kuhakikisha wamiliki wa viwanda wanatengeneza mfumo mzuri wa kuhifadhi maji hayo machafu ili kuunusuru mto huo pamoja na afya za wakazi hao

Kwa  picha zaidi zinozo onosha hali harisi ya mto Yombo.
20171017_173457%257E2


20171017_173508%257E2


20171017_173352%257E2


20171017_173339%257E2



20171017_173320%257E2














Screenshot_2017-11-04-20-10-11
Wananchi wa Yombo kilakala wilayani Temeke waitaka serikali kuongeza magari ya kuzelea taka , haya yameongelewa na wananch hao baada ya uchache wa magari hayo jambo linalo pelekea mrundikano wa takataka  na kusambaa katika makazi ya watu baada ya sehemu iliyo andaliwa kukusanyia taka kufurika wingi wa taka hizo.

Aidha mmoja wa  wananchi hao Bi. Sabrina Komba ameiambia plan media kuwa ukosefu wa magari hayo unasababisha uchafuzi wa mazingira kwa kiasi kikubbwa  hususa ni katika kipindi hiki cha mvua nyingi ambapo maji hubeba taka hizo na kuzisambaza katika makazi ya watu na zingine huingia katika mto yombo ambapo husafirishwa moja kwa moja mpaka baharini.
Screenshot_2017-11-04-20-11-14
Vilevile Bi. Sabrina mesema afya za wakazi hao ziko hatarini kutokana na uchafu huo ambao  unaweza kusababisha magojwa ya mripuko na kupoteza maisha ya wakazi hao hususa ni watoto wadogo wanao cheza michezo yao katika maeneo hayo.

Kwa upande wa mwenyekiti wa mtaa huo Bw.Juma Matari amekiri kuwepo kwa uchafu huo na kudai kuwa  magari yamekua ni changamoto kubwa sana hivyo wapo katika mchakato wa kulitokomeza tatizo hilo na hivi karibuni hali itakua swari na wananchi wataishi kwa amani na afya zao zikiwa njema.

Pia Matari amewata  wananchi hao kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu na kutoa ushirikiano wa hali ya juu kuhakikisha tatizo hilo lina tokomea kabisa ili wakazi waishi katika mazingira masafi na salama kwa afya za wakazi hao.

Hata hivyo suala la usafi wa mazingira limekua changamoto katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam hususa ni katika kipindi hiki cha mvua jambo ambalo linaleta wasiwasi kwa afya za wakazi waishio katika jiji la Dar ea salaam kwa ujumla.


Richa ya mkuu wa mkoa Mh. Paul Makonda kuteua siku ya jumamosi kuwa siku ya usafi katika maeneo yote ya jiji la Dar es salaam siku hiyo imekua haizingatiwi katika baadhi ya maeneo na ndio maana tunaona maeneo mengi yakiwa machafu sana hususa ni katika masoko kama; Buguruni,Tandika, Tandale n.k
Screenshot_2017-11-04-20-10-42

0 comments:

Post a Comment