Na;Neema Edson

Wakazi wa yombo kilakala wilayani Temeke mkoani Dar es salaam wachoshwa na uchafunzi wa mazingira utokanao na viwanda katita mto yombo ambao husababisha uchafunzi wa mazingira pamoja na uchafunzi wa bahari ya hindi kwakua maji hayo hutiririka kuelekea baharini
.
Mmoja wa wakazi katika eneo hilo Bw. Seif Chekwa amezungumza na Umoja blog na kusema kuwa mto huo umekua ukichafuka kutokana na maji machafu yanayo toka viwandani kutiririshwa na kuelekezwa katika mkondo wa mto huo jambo ambolo huchafua mto huo na mazingira kwa ujumla.
Aidha Chekwa amesama maji hayo hutoa harufu mbaya ambo nikero kwa wakazi wanao zunguka mto huo jambo ambalo ni hatari kwa afya ya wakazi hao pamoja na watoto wadogo wanacheza katika maji hayo machafu.
Mbali na hayo Chekwa amedai kuwa kutokana na uchafuzi huo unasababisha ongezo la mbu katika eneo hilo ambao huambukiza ugonjwa wa maralia kwa kiasi kikubwa ingawaje watu wanajitahidi kujifunika vyandarua nyakati za usiku wanapo lala.
Vilevile mto huo awali ulikua ukitumika katika shughuli mbalimbali zinazo wasaidia wakazi wa eneo hilo kama kuchota maji ya kutumia majumbani pamoja na shughuli za kilimo cha mbogamboga katika mashamba yaliyopo katika mbonde la mto huo hivyo shughuli hizo zimekatishwa kutokana na uchafuzi huo.
Pia Chekwa ameiomba serikali kuingilia kati suara hilo ili kukomesha tatizo hilo na kuhakikisha wamiliki wa viwanda wanatengeneza mfumo mzuri wa kuhifadhi maji hayo machafu ili kuunusuru mto huo pamoja na afya za wakazi hao
Kwa picha zaidi zinozo onosha hali harisi ya mto Yombo.





Wananchi
wa Yombo kilakala wilayani Temeke waitaka serikali kuongeza magari ya kuzelea
taka , haya yameongelewa na wananch hao baada ya uchache wa magari hayo jambo
linalo pelekea mrundikano wa takataka na kusambaa katika makazi ya watu
baada ya sehemu iliyo andaliwa kukusanyia taka kufurika wingi wa taka hizo.
Aidha
mmoja wa wananchi hao Bi. Sabrina Komba ameiambia plan media kuwa ukosefu
wa magari hayo unasababisha uchafuzi wa mazingira kwa kiasi kikubbwa
hususa ni katika kipindi hiki cha mvua nyingi ambapo maji hubeba taka hizo na
kuzisambaza katika makazi ya watu na zingine huingia katika mto yombo ambapo
husafirishwa moja kwa moja mpaka baharini.
Vilevile
Bi. Sabrina mesema afya za wakazi hao ziko hatarini kutokana na uchafu huo
ambao unaweza kusababisha magojwa ya mripuko na kupoteza maisha ya wakazi
hao hususa ni watoto wadogo wanao cheza michezo yao katika maeneo hayo.
Kwa
upande wa mwenyekiti wa mtaa huo Bw.Juma Matari amekiri kuwepo kwa uchafu huo
na kudai kuwa magari yamekua ni changamoto kubwa sana hivyo wapo katika
mchakato wa kulitokomeza tatizo hilo na hivi karibuni hali itakua swari na
wananchi wataishi kwa amani na afya zao zikiwa njema.
Pia
Matari amewata wananchi hao kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu na
kutoa ushirikiano wa hali ya juu kuhakikisha tatizo hilo lina tokomea kabisa
ili wakazi waishi katika mazingira masafi na salama kwa afya za wakazi hao.
Hata
hivyo suala la usafi wa mazingira limekua changamoto katika maeneo mbalimbali
ya jiji la Dar es salaam hususa ni katika kipindi hiki cha mvua jambo ambalo
linaleta wasiwasi kwa afya za wakazi waishio katika jiji la Dar ea salaam kwa
ujumla.
Richa ya
mkuu wa mkoa Mh. Paul Makonda kuteua siku ya jumamosi kuwa siku ya usafi katika
maeneo yote ya jiji la Dar es salaam siku hiyo imekua haizingatiwi katika
baadhi ya maeneo na ndio maana tunaona maeneo mengi yakiwa machafu sana hususa
ni katika masoko kama; Buguruni,Tandika, Tandale n.k



0 comments:
Post a Comment