NA REGINA
PETRO
Takwimu
nchini zinaonesha kuwa asilimia 17 ya watoto huzaliwa kabla ya muda wa mimba
kukomaa.taarifa hiyo inetolewa na Waziri wa afya, maendeleo ya jamii, jinsia,
wazee na watoto Ummy Mwalimu.
Waziri Ummy
Mwalimu akiwa anaongea na wananchi.
Waziri Ummy
alisema Wizara yake imekuwa na inaendelea kuchukua hatua mbalimbali huboresha
huduma kwa watoto hao ili kuepusha vifo. Alisema watoto njiti huwa katika
hatari zaidi ya kupoteza maisha kutokana na kutokomaa kwa mapafu,kupoteza joto
la mwili kwa haraka zaidi, kupata mahabukizo ya bakteria, kushidwa kunyonya na
kupata manjano.
Alisema ili
kukabliana na tatizo hilo hatua mablimbali zimekuwa zikitekelewa.
Alizitaja
hatua hizo kuwa ni kuwapatia wajawazito dawa ya kusaidaia mapafu ya mtoto kukomaa
haraka, kuanzisha huduma za mama kangaruu katika ngazi ya hospitali, kununua na
kusambaza vifaa vya kuhudumia watoto njiti wenye matatizo ya kiafya.
‟wizara
inaendelea kutoa mafunzo kwa wahudumu wa afya ya ngazi ya jamii, ili waweze
kutoa elimu kwa wananchi kuhusa masuala mbalimbali ya afya ya uzazi na mtoto
ikiwemo dalili za hatari wakati wa ujauzito,”alisema
Aidha
alisema kwamba ni vyema wanawake wakahudhuria kliniki mapema ili waweze
kutambuliwa matatizo yao na pia kupata elimu mbalimbali ikiwamo haja ya kuwa na
mapumziko ya kutosha



0 comments:
Post a Comment