Wednesday, 16 May 2018

MVUA ZAWA GUMZO JIJINI DAR ES SALAAM


           


  Na Juliani Kasimiri

  Mvua zinazoendelea kunyesha katika mkoa wa Dar es salaam zimeonekana kuwa gumzo kubwa hii ni kutokana na mvua izo kunyesha mara kwa mara,nakupelekea athari kubwa kwa wakazi wa mkoa huo hususani wa maeneo ya mabondeni
Mvua hizo zinatakribani wiki moja tokea zianze kunyesha katika maeneo mengi mkoa humu,lakini zimeonekana kuwa na athari kubwa za kiuchumi na kimiundombinu.
Hussain Bakari ni mfanyabiashara katika soko la buguruni,kwa upande wake mvua hizo zimemfanya ashindwe kufanya biashara zake za kupanga mboga mboga hii ni kutokana na kunyesha mara kwa mara kwa mvua hizo.


Asha Mussa ni mkazi wa buguruni yeye anaona mvua hizo zimefanya usafiri kuwa mgumu hususani anapotaka maeneo yake ya kazi kuelekea nyumbani.

Ata ivyo watu mbali mbali katika mkoa huo wameonekana kuendelea na shughuli zao za kujipatia kipato,licha ya mvua hizo kuendelea kunyesha katika maeneo mengi jiji hapa. 

0 comments:

Post a Comment