Wednesday, 16 May 2018


Na;Saraphina Shanes
Screenshot_2017-09-26-14-39-03 
  


 Wananchi wa jiji la Daressalaam wameiomba serikali kutilia mkazo suala la usafi katika siku ya jumaamosi ambapo wananchi hao wameiomba serikali ihakikishe watu wote wanafanya usafi katika mazingira badala ya kujifungia ndani hadi mda wa saa nne unapofika ndio wanafanya shughuli zao jambo ambalo limeonekana lipo kinyume na Agizo la mkuu wa mkoa Mh.Paul Makonda linalowataka watu wote wa jiji hilo wafanye usafi
Wananchi wa jiji hilo wamekuwa na mitazamo tofauti kuhusiana na usafi,ambapo baadhi yao wamesema  kuweka mazingira safi  ni jukumu la kila mwanachi, wapo waliosema kuwa mda uliowekwa sio rafiki hivyo ni bora mda ukapunguzwa baada ya mwisho saa nne  iwe saa tatu kutokana na mda wa masaa mawili yaani saa kumi na mbili hadi saa mbili ni muda unaotosha kufanya usafi.
Katika mahojiano na baadhi ya wananchi mwandishi wetu alifanikiwa kuongea na mkazi wa Ilala jijini Daressalaam Ndugu Joseph .K. Christopher:”Alisema kuwa ni kweli wanajua suala hili ni zuri kwa jamii kulifuatilia na kuhakikisha kila mmoja anafanya usafi kwenye eneo aliopo ili kuepusha magojwa ya mlipuko kama kipindupindu na Kuhara.
Akiongeza ndugu Joseph .K. Christopher amesema serikali inalengo zuri na nchi yetu hasa jiji hili la Daressalaam amabalo watu wa nchi  mbalimbali wanalitembelea,Pia uwepo wa Wizara muhimu jambo ambalo linatakiwa kufanya jiji kuwa safi na kuendana na hadhi yajiji lenyewe kuwa la kimataifa.hayo yalisemwa na mkazi huyo.
Pia mwandishi wetu alipata  kuongea na mmoja wa wafanya biashara Ndugu Said Sanze ambae ameipongeza serikali pamoja na kusema kuwa ni sawa kabisa kutenga siku ya usafi na ikiwezekana ziongezwe siku na kufanya sikuzote ziwe za usafi na kuweka wasimamizi ambao watafuatilia kwa ukaribu  hili suala ili kuhakikisha kwa wale watakaoenda kinyue na sheria wanachukuliwa hatua za kisheria.
Mwisho ni maoni ya wananchi wa Daressalaam ambapo kwenye mahojiano na mwandishi wetu raia  wameishauri serikali iongeze nguvu kwenye suala hili kwa kutoa elimu kwa wananchi jinsi gani hii siku ilivyo na umuhimu na pia waelezewe kuhusu faida ya kuweka mazingira safi,Pia wamewaomba wananchi waishio jiji hilo kuachana na zana ya kuwa wanaotakiwa kufanya usafi ni wafanya biashara pekee badala yake watoe ushirikiano katika kuhakkisha jiji linakuwa safi.





0 comments:

Post a Comment