Wednesday, 16 May 2018


Na;Saraphina Shanes

CHANGAMOTO za maisha ni njia ya mafanikio kwa binaadamu hivyo ndivyo ilivyo na hakuna anaepingana na huu ukweli ambao umedhihirishwa na kijana wa kitanzania Bwana Omari Hafidhi ambae amepitia mengi katika safari yake ya maisha,ambae anahistoria ya pekee baada ya kupanga vyumba takribani 15 kwa nyakati tofauti lakini  sasa ni moja ya vijana walio na msaada mkubwa kwa vijana wengine.

Omari Hafidhi ni mzaliwa wa Pemba kaskazini,amezaliwa mwaka 1980 katika Hospitali  ya wete,ambapo katika upande wa mama yake yeye ni motto wa 6 na upande wa Baba ni mtoto wa 5,katika familia yao alikuwa akilelewa na mama pekee,ambapo Omari alianza kujihusisha na shughuli  ndogndogo za kujipatia kipato akiwa na umri wa miaka kumi na mbili[12]ili kuisaidia familia.

Alipofikisha umri wa miaka kumi na tano[15]alienda mjini Unguja ambapo alikuwa akijihusisha na kazi ya uvuvi kwa mda wa miaka isiyopungua sita,na baada ya hapo alienda jiji la Daresalaam mwaka 2000 ambapo alikuwa akifanya biashara ya kuuza matunda akiwa kama mchuuzaji,alifanya biashara hiyo kwa mda wa mwaka mmoja na hatimae alirejea tena Pemba.

Alipokuwa pemba alipatwa na tatizo la kupigwa na lisasi ya mguu baada ya vuguvugu la maandamano ya kisiasa yaliyotokea  2001ambapo alisaidiwa na wasamalia wema na kumpeleka hospitali ya Mnazi mmoja iliyopo Zanzibar na bnaadae alihamishiwa Daresalaam kwa matibabu zaidi katika hospitali ya Muhimbili,baaada ya hali ya kiafya kuimalika omari aliruhusiwa kutoka hospitali hapop.

Aliporuhusiwa alikuwa akiishi na mjomba wake Temeke ambapo al;ikuwa akifanya biashara ya kuuza juisi katika mgahawa wa mjomba wake,na baadae alihamia bugurni ambapo alipata kufungua mgahawa wake wa kuuzia juisi baada ya kupewa pesa na kiongozi mmoja wa chama wa kisiasa alipokuwa anahitaji nauli ya kiasi cha fedha tasiliumu za kitanzania shilingi 150,000 ili arudi kwao lakini akaona kama fursa na baadae aliitumia pesa kuanzishia biashara yake ya juisi.

Omari alifanikiwa kuiendeleza biashara yake ya juisi na haimae alifanikiwa kuwaajili vijana wa kazi wasiopungua 26,ambapo aliongeza vitu v1ya biashara na alikuwa akiuza vyakula mbalimbali pamoja na vinywaji ambapo alikuwa amefungua Café iliyomuinua zaidi kimaisha na hatimae alifanikiwa kununua gari mbili za abiria aina ya Costa,viwanja viwili chin na vingine Pemba,pia amefanikiwa kujenga nyuma mbili ambapo zilizopo buguruni ambazo zina thamani kubwa.


Pia omari amefanikiwa kumlea mtoto wa kaka yake aliefariki 2006,kwa sasa amefanikiwakumlea mtoto huyo ambaye kwa sasa yupo kidato cha sita,pia omari ana watoto watano[5]ambao anaishi nao,pia hadi sasa amekuwa akiendelea na biashara yake ya juisi ambayo imekuwa ni chachu kwenye mafanikio yake,






0 comments:

Post a Comment