Wednesday, 16 May 2018



Na;Neema Edson


image%2B%25281%2529
Mto Msimbazi umeacha njia yake na kujitengenezea njia nyingine katika eneo la Vingunguti jijini Dar es Salaam hali iliyosababisha baadhi ya nyumba kubomoka na kuhatarisha usalama wa nyumba nyingine pamoja na usalama wa wakazi wa maeneo hayo.
Katika eneo la JANGWANI, Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya DSM limelazimika kufunga barabara katika eneo hilo ili kunususru usalama wa watu na pia kulazimu huduma ya mabasi yaendayo haraka kusitisha safari zake.
Katika eneo la Jangwani Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limelazimika kufunga barabara eneo hilo ili kunusuru usalama wa watu na pia kulazimu huduma ya mabasi yaendayo haraka kusitisha safari zake.
PMTV imeshuhudia baadhi ya wakazi wa Jiji wakilazimika kuvuka katika eneo la Jangwani ili waweze kuendelea na shughuli zao za kila siku. 
Eneo la Jangwani ni kati ya meneo ya jiji la Dar es Salaam ambapo Mto Msimbazi unapita na kuleta madhara makubwa kwa wakazi wanaoishi karibu na mto huo, yakiwemo ya nyumba zao kujaa maji kipindi cha mvua.
Kwa ujumla mvua zilizonyesha kwa takriban siku mbili mfululizo hadi jana zimeleta adha kubwa katika baadhi ya maeneo ya jiji la Dar es Salaam hali iliyomlazimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kufika eneo la Vingunguti na kutoa tahadhari kwa wakazi wa eneo hilo wanaoishi karibu na Mto Msimbazi.
Makonda amewataka wakazi wa Dar es Salaam kuchukua tahadhari kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini.








0 comments:

Post a Comment