Wednesday, 16 May 2018

UPIMAJI WA UKIMWI NA KIFUA KIKUU (TB) BAA SIO LAZIMA.

NA REGINA PETRO
Waziri wa afya, maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto, Ummy Mwalimu amesema upimaji wa kifua kikuu(TB) na ukimwi kwenye baa hautakuwa wa lazima .






Waziri Ummy Walimu waliutumia wananchi.
Akizungumza wakati wa maadhimisho wa miaka 30 ya mpango wa Taifa wa kudhibiti ukimwi (NACP), Mwalimu alisema baada ya kutolewa taarifa ya kuwepo mpango huo watu wengi wamekuwa na hofu. ‟Tutatekeleza mpango wa kusogeza huduma za upimaji TB na ukimwi kwenye naa, ila hautakuwa wa lazima, tuachofanya ni kuwashawishi wananchi kutumia fursa ya kusogezewa huduma hiyo,’’
 
Upimaji kwa hiari wa mtu mmoja mmoja .
Aidha, alisema kwa sasa wizara yake iko kaktika mkakati wa kufanyaia marekebisho ya sharia ya Ukimwi kwa lengo la kuruhusu watu kujipima mwenyewe, kutoa fursa kwa vijana kuanzia miaka 15kwenda kupima ukimwi bila kupata ridhaa ya wazazi ay walezi.
Katika hatua nyingine,Mwalimu aliagiza kuanzia Julai mosi mwaka huu, watu wanaoishi na virusi vya ukimwi kupewa dawa za miezi mitatu badala ya sasa ya kupewa kwa miezi mwili. Agizo alilitoa kutokana na Mwenyekiti wa baraza la watu kudai kuwa utaratibu wa kupewa dawa za miezi miwili umekuwa ukiongezea gharama,kwani wamekuwa wakitakiwa kupima afya zao kila baada ya miezi mitatu. Waziri huyo alisema utaraibu huo wa kuwapa dawa miezi mitatu mitatu uanza haraka isipokuwa kwa wale ambao wanaonekana hawataweza kutuza dawa hizo au ambao ndio kwanza wanaznza kutumia dawa hizo.
 

0 comments:

Post a Comment