Na Jacqueline Benson
KISUKARI aina ya ugonjwa unaoendelea kutajwa kusumbua watu wengi hususan wenye kipato cha
juu. Sababu za ugonjwa huo zinaelezwa na wataalamu lakini zimekuwa zikipuuzwa
huku wanaosema ugonjwa huo ni wa watu
wenye kipato cha juu wakizidi kuangamia pasi na kujua.
Hiyo inaifanya idadi ya watu wanaopoteza maisha
kuongezeka ambapo kwa mujibu wa Wizara ya Afya, Maendelo ya Jamii, Jinsia Wazee
na Watoto kwa mwaka 2005 kati ya vifo milioni 58 vilivyotokea watu miilioni 35
walifariki kwa magonjwa yasiyoambukiza na huku magonjwa hayo yakizidi kuongezeka hasa hapa nchini .
Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa NIMRI kwa mwaka 2012
ilitoa ripoti ya ongezeko la visababishi vya magonjwa yasiyoambukiza. Utafiti
huo unaonyesha uvutaji wa sigara unachangia magonjwa yasiyoambukiza kwa
asilimia 15.9 unywaji pombe kwa asilimia 29 wanaotumia matunda na mbogamboga
mara tano kwa wiki asilimia 97 wanene kupitiliza asilimia 26 wanaotumia mafuta
mengi asilimia 35 na shinikizo la damu asilimia 25.
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa
mwaka 2015 inakadiriwa watu milioni 1.6 wanakufa kutokana na ugonjwa wa
kisukari. Daktari Bingwa Matibabu Ugonjwa wa kisukari na Homoni Banduka
Elisante alisema ugonjwa wa kisukari
unatokana na kuongezeka kwa
kiwango cha sukari katika damu na kusababisha mfumo wa unaodhibiti
sukari mwilini kushindwa kufanya kazi


0 comments:
Post a Comment