Na Shani Seif
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amewaonya
wasichana wa mkoa wake wa Dar es salaam kutokubali kuolewa na wanaume wanaoishi
katika maeneo ya bondeni ambayo ni hatarishi hasa katika kipindi cha mvua za
masika.
![]() |
| Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam |
Makonda amesema hayo alipofanya ziara katika eneo la mbagala kiburugwa na kuona baadhi ya nyumba za wananchi ambazo zimeathirika kutokana na kujengwa katika maeneo hatarishi na kuwataka wakazi hao kuhama mara moja.
Makonda ameongeza kuwa serikali haitaweza kutoa msaada wa chakula na malazi kila mara kwa wananchi ambao wanakumbwa na majanga yanayotokana na wao kuamua kukaa katika maeneo hatarishi kwa kujitakia.
![]() |
| Baadhi ya wakazi wanaokaa mabondeni |
Mkuu wa mkoa huyo amedai kuwa maeneo hayo ni
ngumu kwa mwananchi kupata msaada wa dharura ikiwemo gari la wagonjwa au huduma
ya zima moto.


0 comments:
Post a Comment