Wednesday, 16 May 2018

DANGOTE AKABIDHI SARUJI MKOANI MTWARA.

Na. Maua Patrick.

Kiwanda cha uzalishaji wa saruji cha kampuni ya Dangote kimetoa mifuko 2400 ya saruji kwa mkuu wa mkoa wa mtwara kwa ajili ya ujenzi wa maendeleo ya madarasa , vyoo pamoja na nyumba za walimu kwa shule za halmashauri ya manispaa Mtwara.


Amezungumza na CHIPUKIZI Kaimu Katibu Tawala wa wilaya ya Mtwara FRANSICS TRIPHONY MKUTI ameeleza kuwa mifuko ya saruji kutoka kwa Mwezeshaji Dangote itakidhi mahitaji na kuwezesha ujenzi huo kwa asilimia kubwa.

“Tunaomba wawezeshaji wengine wajitokeze ili tuweze kuendesha hili suala la utengenezaji wa madarasa na vyoo vya kila shule wilayani Mtwara kwa wepesi zaidi. hakika mifuko tuliyopokea kutoka kwa Dangote itakidhi mahitaji kwa asilimia kubwa katika ujenzi na kubaki na vitu vidogo vidogo” Alisema Mkuti


Pia FUNDIKILA MASAMALO akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Mtwara amesema kuwa anahaidi kutumia mifuko ya saruji hiyo na kukamilisha ujenzi ipasavyo ili watoto wapate kusoma kwa usalama zaidi kwa mazingira safi na ulinzi wa afya zao.

0 comments:

Post a Comment