Wednesday, 16 May 2018



Na;Neema Edson
Screenshot_2017-11-04-15-05-35
Wakazi na watumiaji wa barabara inayo unganisha Buguruni kwa mnyani na Vingunguti machinjioni  jijini Dar es salaam wapaza sauti zao baada ya kukutana na kamera ya Plan Media wakilalamikia ubovu wa barabara hiyo na kuiomba serikali kuiboresha barabara hiyo ambayo imegubikwa na ubovu kwa muda mrefu pasipo kuikarabati.

Aidha barabara hioyo ina mashimo mengi pamoja na kujaa maji katika mashimo hayo kutokana na mvua zinazo endelea kunyesha jambo ambalo linasababisha wananchi hao kuitumioa kwa taabu na kusababisha foreni ya magari amboyo huwasababishia watu kuchelewa katika safari zao.
Screenshot_2017-11-04-15-06-07


Screenshot_2017-11-04-15-06-12

Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wananchi hao walikua na haya yakusema, Bw. Shaaban Songo ambae ni kondakta wa gari la abiria linalo fanya safari zake kati ya Vingunguti na Mnazimmoja amesema barabara hiyo imekua kero sana ambapo husababisha magari yao kuharibika marakwamara kutokana na mashimo ya barabara hiyo.

Vilevile Bi.  Maryam Marwa ambae ni mkazi wa Vingungunti dereva wa gari binafsi amesema wanalazimika kubuni njia za vichochoroni  wakihofia kuharibika kwa magari  yao huku wakiingia garama kubwa ya mafuta pamoja na muda kwasababu huwapasa kutembea taratibu sana.

Kwa upande wa  Bw.Hasheem Mhina ambae pia ni mkazi na mfanya biashara wa vingunguti amesema wanapata shida kupitisha mizigo yao kwa kutumia magari makubwa ya mizigo wakihofia kuzama kwa magari hayo kwasababu ubovu huo unatisha mno.

Pia Bw. Husien Mpilaru ambae ni serikali ya mtaa amesema anafahamu ubovu wa barabara hiyo na kuiambia plan media kwamba babara hiyo haiko chini ya manispaa ya ilala bali ipo chini ya TAKULA ambao walitakiwa waitengeneze tarehe 5/10/2017 huku mpaka leo hakuna dalili za TAKULA kuitengeneza barabara hiyo.
Screenshot_2017-11-04-15-06-37
Vilevile Mpilaru ameongeza na kusema kuwa anaiomba serikali kuja kuiangalia barabara hii na kuifanyia ufumbuzi ili kuiondoa kero hii ya muda mrefu ili wakazi hao waitumie kwa amani katika shughuli zao mbalimbali ikiwemo usafirishaji katika kujenga taifa.

0 comments:

Post a Comment