Friday, 18 May 2018

WANAFUNZI WAJITOKEZA KATIKA ZOEZI LA KUPIGA KURA

Na Shani Seif

Mchakato wa Uchaguzi   unafanyika siku hii ya leo katika chuo cha Uandishi wa habari cha TIME SCHOOL OF JOURNALISM TSJ . Wanafunzi chuoni humo wanafanya zoezi  la kupiga kura la kuchagua viongozi ngazi ya Urais na makamo wa urais.

Uchaguzi umesimamiwa kikamilifu na walimu ,mwenyekiti wa tume pamoja na viongozi ukizingatia usalama na utulivu wa wanafunzi kufanya zoezi hilo bila vurugu.


Mmoja wa wanafunzi akipiga kura
Wanafunzi wakijiandaaa kupiga kura

Chumba cha kupigia kura


Aidha wanafunzi wameonekana wakifanya zoezi hilo la kupiga kura kwa utulivu huku wakiwa na shauku kubwa ya kusubiri matokeo ambayo yanatolewa siku hii ya leo baada ya zoezi la kupiga kura kukamililka

0 comments:

Post a Comment