Na.Edward Benson.
Mvua zinsazo fururza kunyesha
katika jiji la Dar es salaam zimesababisha kuwakwamisha wakazi na watumiaji wa
barabara ya morogoro road baada ya daraja la kibanda cha mkaa lilipo maeneo ya
mbezi kufurika maji nakusababisha shughuli za usafirishaji kukwama kwa muda
katika barabara hiyo.
Aidha mvua hizo ambazo zimefururiza
kwa siku mbili zimeendelea kusababisha uharibifu wa miundombinu ya barabara na
majumba katika eneo hilo la mbezi wakati huo mvua ikiendelea kunyesha jambo
ambalo linaleta hofu kwa wakazi wa eneo hilo.
Vilevile wakazi wa eneo hilo akiwemo
ndugu. Jonasi Razaro amesema kuwa mvua hizo ambazo zinaendele kunyesha
zinaendele kufanya uharinifu mkubwa katika eneo lambezi hususa ni katika maeneo
ya kibanda cha mkaa.
Pia Razaro ameongeza kwa kusema kuwa
mvua kama zitaendelea kufururiza namna hii basi yatatokea maafa makubwa zaidi
hivyo wale wanao ishi mabondeni katika eneo la kibanda cha mkaa na maeneo
mengine ni heri wakachukua tahadhari mapema kabla maafa hayajawafika.
Hata hivyo mvua hizo zinazo endelea
kunyesha katika jiji la Dar es salaam zinaendelea kusababisha mafuriko katika
maeneo mbalimbali ya jiji hilo hali yakuwa ni kawaida kwa mafuriko kutokea marakwara
pale tumvua inapo nyesha.
Mamlaka ya hali ya hewa enaendelea
kutoa tahadhari kwa wakazi waishio mabondeni kuchukua tahadhari kabla maafa
hayajawakuta huku baadhi ya wakazi wakiwa wagumu wa kutii tahadhari hiyo inayo
tolewa na marakwamara,

0 comments:
Post a Comment