Wednesday, 16 May 2018

MASHIMO YAWA KELO KWA MADEREVA BARA BARANI


        
  Na Juliani Salvatory.

       Kuongezeka kwa mashimo katika Bara bara nyingi mkoani Dar es salaam kumeonekana kuwa ni kelo kubwa kwa madeleva watumiao bara bara hizo.
Licha ya Serikali kutumia gharama kubwa katika utengenezaji na ukarabati wa miundombinu hiyo ya bara bara,lakini bara bara hizo zimeonekana kuwa chini ya kiwango kinachopelekea kuwa na mashimo mengi katika jiji la Dar es salaam.
Sadam Jumanne ni dereva boda boda maeneo ya buguruni,kwa upande wake anaona mashimo hayo yamezidi kuwa mengi  na kuiomba serikali kuchukuwa hatua katika kukarabati miundombinu ya bara bara hizo.
Bakari Simi yeye ni dereva wa dala dala ziendazo Buguruni-Makumbusho,kwa upande wake anaiomba serikali kuchukua juhudi za haraka katika kukarabati mashimo hayo kwani upelekea ubovu wa vyombo vyao vya usafiri.
Wakandarasi wanaopewa tenda ya kutengeneza miundombinu ya bara bara wanapaswa kutengeza bara bara zenye ubora na zinazokidhi maitaji ya watumiaji wa bara bara hizo,kwani itasaidia kuepusha ajali mbali mbali zisizo na hulazima.  

0 comments:

Post a Comment