Wakazi
wa buguruni mkoani Dar es salaam walalamikia ongezeko la ada ya uzoaji wa taka
kutoka shilingi elfu tano (5000) hadi shilingi elfu saba (7000) katika hali
isiyo ya kawaida wakazi hao walalamikia serikali ya mtaa huo kwa ongezeka hilo
la shilingi elfu mbili (2000).
Wakati wa mahojiano na mwandishi wetu wakazi hao wameiambia umoja blog kuwa mbali na ongezeko la ada hiyo wamekua wakicheleweshewa gari za kubebea
takataka ambapo inapelekea kuwepo kwa mrundikano wa takataka ambazo
husababisha madhara kiafya
Umoja
blog ilimtafuta mwenyekiti wa mtaa Ndugu.Karim Marapa alisema kuwa nikweli ada
imepanda katika uzoaji taka ikiwa ni makubaliano ya serikali ya mtaa pamoja na
wananchi wake.
Aliendelea kuzungumza ndugu Marapa kuwa wananchi wananchi wanatakiwa kuwa na uvumilivu na serikali yao kwani kero zao zinafanyiwa kazi hivyo ni vizuri wakatoa ushirikiano ili kuisaidia serikali kuwatimizia yale waliyo waahidi.
Aliendelea kuzungumza ndugu Marapa kuwa wananchi wananchi wanatakiwa kuwa na uvumilivu na serikali yao kwani kero zao zinafanyiwa kazi hivyo ni vizuri wakatoa ushirikiano ili kuisaidia serikali kuwatimizia yale waliyo waahidi.
Mwisho kabisa ni maoni ya mwananchi ambapo mwandishi wetu alipata kuzungumza na Ndugu.Beshe Buhira ambae ni mkazi wa mtaa huo alisema kuwa anawaomba wahusika wa ukusanyaji wa takataka katika mtaa huo waongeze bidii katika kazi yao ili kuhakikisha wanajenga uhusiano mzuri na wananchi.
0 comments:
Post a Comment