Na. Maua Patrick.
ELIMU
imeendelea kutolewa ili kuhakikisha mfumo huu wa ulipaji wa kodi ya pango la ardhi
kwa njia ya kielektroniki unakuwa na tija.
Serikali
kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, imeanzisha mpango wa
kutoa mafunzo kwa kuteua kikosi kazi kinachotoa mafunzo juu ya matumizi ya
mfumo huo.
Hatua
hiyo imefikiwa ili kuelimisha mikoa mingine baada ya kupata mafanikio mazuri
katika mkoa wa Dar es Salaam na Pwani, kwa watendaji
wote wa sekta ya ardhi.
Miongoni mwa njia kuu na muhimu kwa nchi
kujipatia maendeleo ni kuzingatia ulipaji wa Kodi.
Serikali imezingatia suala hili kwa kuboresha mifumo
ya ukusanyaji malipo mbalimbali malipo
ya ndani.

.
OfisakutokaWizarayaArdhi, Nyumba naMaendeleo ya Makazi Haruna Kiyungi, akieleza
jinsi ya kutumia Mfumo waulipa kodi ya pango la ardhi kwanjia ya kielektroniki.
Kwa hatua ya kwanza ilizindua mfumo wa ukusanyaji
Mapato wa Serikali kwa njia ya kielektroniki (e-RCS), uliotengenezwa na Mamlaka
ya Mapato Tanzania (TRA) na Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) kwa
kutumia wataalamu wa ndani.
Akizindua mfumo huo katika Kituo cha Taifa cha Kuhifadhi
Kumbukumbu (NIDC), kilichopo Kijitonyama, Rais Dk. John Magufuli, alisema “Wanaokusanya
mapato wanalalamika kuwepo kwa udanganyifu kwenye utoaji taarifa za
wafanyabiashara.
Ofisa
Ardhi David Malisa (katikati) akitoa mafunzo kwa Maofisa kutoka Ofisi ya Kamishna
Msaidizi wa Ardhi kanda ya Ziwa jinsi ya kutumia Mfumo wa GePG.
Wafanyabiashara nao wanalalamika kubambikizwa
kodi, sasa dawa ya haya yote yatatatuliwa na uwepo wa kituo hiki, jiungeni na
mfumo huu kwani kila kitu kinafanywa na mashine, hakuna kuonea mtu,”.
Kwa maana
hiyo, serikali imeamua kuboresha mfumo wa ukusanyaji wa maduhuli kuwa wa
kielektroniki, ili kurahisisha ukusanyaji wake na kuongeza uwazi miongoni mwa
wizara na taasisi mbalimbali za serikali.
Aidha, kwa upande wa malipo
ya kodi ya pango la ardhi, dhana ya ulipaji wa kodi hiyo inatokana na Sheria ya
Ardhi namba 4, ya mwaka 1999, fungu la 3, kifungu kidogo cha 1(a).
Wizara ya Ardhi, Nyumba
na Maendeleo ya Makazi kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha na Mipango, zimedhamiria
kuboresha malipo ya ukusanyaji kodi ya pango la ardhi kwa kutumia mfumo wa
kielektroniki wa ‘GePG’.
Mfumo huo
utahusika katika makusanyo ya kodi ya pango la ardhi pamoja na tozo zingine
zinazotokana na sekta ya ardhi nchini.
Hivi karibuni mfumo wa ulipaji kodi ya pango la ardhi
kwa njia ya simu ya mkononi umeanza
kutumika Wizara ya Ardhi kwa makusanyo ya pango la ardhi.
Mfumo huo, unawarahisishia mwananchi kulipia
popote alipo kwa kutumia tovuti ya wizara au simu za mkononi kwa wananchi wanaomiliki
viwanja au mashamba yaliyopimwa.
Watapatiwa hati maalum ili ku ataweza kutumia
simu yake ya mkononi kuona kiasi cha kodi ya pango la ardhi anachodaiwa na
kulipa kwa kutumia simu yake ya mkononi.
Kaimu Katibu Mkuu,
Wizara ya Ardhi Dk. Moses Kusiluka, anazungumzia utaratibu wa mapato ya kodi ya
pango la ardhi kwa njia ya kielektroniki na kueleza uamuzi wa kufunga akaunti
za kukusanyia kodi hii, kupisha mfumo mpya.
Dk. Kusiluka anawatahadharisha
wamiliki wa ardhi wenye hati au hati maalumu ijulikanayo kwa jina la ‘ofa’,
kuhakikisha wanalipa kodi hiyo kwa wakati, vinginevyo muda wa malipo ukipita
watatozwa faini ambayo wasipolipa baada
ya siku 14 watapelekwa mahakamani.
Anasema ili mwananchi
kujua anadaiwa kiasi gani cha kodi ya pango la ardhi kwa kutumia simu ya
mkononi, anatakiwa kubonyeza *152*00# kuandika ujumbe na kutuma kwenda namba
15200.
Baada ya hapo anaweza
kulipia kwa njia ya mitandao ya simu na benki.
Anaeleza huduma zingine
za sekta ya ardhi, zinazohusisha malipo hayo ni tozo mbalimbali za sekta ya
ardhi ikiwemo upekuzi katika daftari la msajili, ambapo mwananchi
atapaswa kutembelea ofisi za wizara zilizopo katika eneo lake.
Baada ya hapo atapatiwa
makadirio ya kulipia huduma husika pamoja na namba ya malipo itakayomuwezesha
kulipia kwa njia ya benki na simu ya mkononi.
Kwa mmiliki wa ardhi
iliyopimwa na kupatiwa hati ya umiliki, Kaimu Katibu Mkuu huyo anasema anaweza
kuulizia kiasi cha fedha anayodaiwa na kulipia kodi husika.
Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Dk.
Shaaban Pazi, anabainisha kwamba mfumo wa GePG, ulianza kutumika rasmi Juni,
mwaka huu.
“Mafunzo ya awali yalitolewa kwa ofisi ya Dar es
Salaam na maeneo mengine, mfumo huu ni rafiki kwani utaboresha na kurahisisha
ukusanyaji wa malipo ya kodi ya pango la ardhi.
Mkurugenzi wa mifumo ya kifedha Wizara ya Fedha na
Mipango, John Sausi, anasema njia ya ulipaji wa kodi hiyo kwa mtandao
utaiongezea serikali makusanyo ya kodi kwa wakati.
“Kutokana na makusanyo
hayo kwenda moja kwa moja kwenye akaunti ya serikali, itaondoa msongamano wa
watu waliokuwa kwenye utaratibu wa awali wa ulipaji kodi.
Uanzishwaji wa mfumo
huo utaenda sawia na utoaji elimu ya matumizi kwa wananchi ili waweze
kujihudumia kwa haraka na uhakika,” anasema.
. Maofisa
kutoka Ofisi ya Kamishna Msaidizi wa Ardhi Kanda ya Ziwa wakijifunza jinsi y akutumia
mfumo huo.
Halima Chitemi, mkazi
wa Dar es Salaam, akiwa katika foleni ya
kufanya malipo ya kodi hiyo wizarani, baada ya shighuli ya utoaji elimu, hakuwa
tayari kuanza kufanya malipo hayo kwa njia ya simu akihofia kutofanikiwa
kukamilisha malipo hayo.
Hata hivyo Adam Manase,
ambaye akiwa kwenye foleni hiyo, alikubali kufanya malipo hayo kupitia simu
yake na kufanikiwa vema huku akiwaacha waliohofia kutumia njia hiyo wakisubiri
kwenye foleni.
Mkuu wa Kitengo cha
Kodi, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dennis Masami,
anawahamasisha wananchi kutambua mabadiliko ya utaratibu wa ulipaji kodi hiyo.
Badala ya watu kufika wizarani
kwa ajili ya kufanya malipo ya kodi ya pango la ardhi, hivi sasa wafanye kwa
nija ya kielektroniki.
“Kwanza mtu ataweza kufanya makadirio ya madeni
yake kwa njia ya simu au kupitia tovuti ya serikali na kulipia kwa njia ya mtandao
au benki husika jambo litakalosaidia kuokoa muda,” anasema.
Masami anaeleza licha
ya mfumo wa kielektroniki kurahisisha ulipaji wa kodi hiyo, pi utawezesha
malipo kufanyika kwa usalama zaidi na kuzuia mianya ya utapeli.
Changamoto kadhaa
zimejitokeza ambazo wizara imebaini na inaendelea kuzifanyia kazi ikiwemo kundi
la watu wasioweza kufanya malipo hayo kwa kutomiliki simu na kukosa huduma ya mtandao katika maeneo yao.
“Wizara inaandaa
utaratibu wa kusajili vipande vyote vya ardhi ili wamiliki wote wa ardhi ya mijini
ambao hawajasajiliwa, wasajiliwe ili wahusike kulipa kodi hiyo.
Pia lipo kundi la
wamiliki wa ardhi kadhaa wanaofanya malipo hayo kielektroniki na kuhitaji
risiti za karatasi, zaidi ya zinazopatikanika kwenye simu ambapo hulazimika kufika
kwenye ofisi ya halmashauri husika,” anasema.
Anasema ujenzi wa kituo
cha mfumo wa kielektroniki wa kumbukumbu za ardhi umeanza kutekelezwa, ukikamilika utaboresha
uwekaji wa kumbukumbu za wamiliki wa ardhi na hivyo kurahisisha ukusanyaji wa
kodi za ardhi kwa ubora zaidi.
Ujenzi wa jengo la kituo
cha mfumo wa kielektroniki wa kumbukumbu au uhifadhi wa taarifa za ardhi, kwa
sasa umekamilika na kitajulikana kwa jina la ‘Kituo cha Taifa cha Taarifa za
Ardhi’.
Ni matumaini wizara
itazingatia weledi katika ukusanyaji wa kodi ambazo kimsingi zitatumika kuleta
maenbdeleo ya taifa.
Pia elimu zaidi
iendelee kutolewa kwa wananchi juu ya umuhimu wa ulipaji kodi na matumizi ya
njia ya kielektroniki.
000


0 comments:
Post a Comment